Saturday, October 18, 2014

Baada ya Miss TZ 2014 kuandamwa mitandaoni, Miss TZ wa 2013 ameamua kuyaandika haya


Kama na wewe unakerwa au haupendi jinsi ambavyo Miss Tanzania wa 2014 Sitti Mtemvu amekua akiandamwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu umri wake na elimu yake baada ya kushinda taji hilo weekend iliyopita basi uko upande mmoja na Miss Tanzania wa 2013 Brigitte Alfred.
Kupitia page zake za twitter na Instagram Brigitte pamoja na mengine ameandika >>> ‘ Mazuri mengi yanawapita lakini inapotokea skendo mnajadili milele ndio maana hatuendelei, natamani tungeweka hizi nguvu za matusi kwenye vitu vya kujenga‘
Baada ya hiyo sentensi Brigitte alimuandikia Sitti kwa kusema >>> ‘Sitti usiwaruhusu watu wakuandame sana, ikizidi warudishie tu taji lao’

No comments:

Post a Comment