Wednesday, December 17, 2014

Ile issue ya Escrow, hii ni taarifa ya Kiongozi mmoja kujiuzulu

Wiki chache zilizopita wakati Kikao cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kikiendelea, macho ya watu wengi na masikio yalikuwa na hamu ya kutaka kuujua mwisho wa sakata la Escrow.
Wakati watu wengi wakisubiri maamuzi yatakayotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete kuhusiana na Ripoti juu ya issue ya ubadhilifu wa fedha kwenye akaunti ya Escrow, leo December 16 kuna taarifa iliyotufikia muda mfupi iliopita kuhusu kiongozi mmoja wa Serikali kujiuzulu.
WeremaTaarifa iliyoripotiwa na kituo cha ITV inasema aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amejiuzulu siku ya leo na barua yake tayari imefika Ikulu ambapo Rais Kikwete ameridhia maamuzi hayo na kumshukuru kwa uamuzi huo kwa kuwa ushauri wake kuhusiana na suala la Tegeta Escrow haukueleweka.

No comments:

Post a Comment