Saturday, December 19, 2015

TAASISI 1,200 DUNIANI ZAMPA TUZO YA AMANI EDWARD LOWASSA


Taasisi 1,200 duniani zitampa aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa Tuzo ya Amani kutokana na utulivu aliouonyesha kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu.
Akizungumza na Mwananchi kutoka Bukavu, DR Congo, mwenyekiti wa Kamati ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii, Mchungaji William Mwamalanga alisema Lowassa amechaguliwa jana mjini Bukavu na wajumbe 1,400 wa mkutano huo.
Mwamalanga alisema wajumbe wanaohudhuria kongamano la amani wanatoka mataifa ya Ulaya, Marekani, Asia na Afrika kwa kuwashindanisha wanasiasa 1,000 ili kumpata Kiongozi Bora wa Amani mwaka 2015, ambaye anajali na kuangalia maslahi ya jamii badala ya madaraka

No comments:

Post a Comment